Thursday, 27 March 2014

JUHUDI ZA KUMUOKOA MTOTO MWENYE RISASI KICHWANI{KENYA}

Mtoto aliyejeruhiwa na risasi iliyomuua mama yake katika shambulio lililofanywa kwenye kanisa la JOY OF JESUS Lililoko mjini Mombasa Nchini Kenya tukio lililotokea siku ya jumapili, amefikishwa jijini Nairobi kwa Ndege tayari kwa upasuaji.
Satrin Osinya mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu anatarajiwa kufanyiwa upasuaji wa kichwa katika Hospitali kuu ya Kitaifa ya Kenyatta ili kuondoa risasi hiyo iliyoingia kwenye ubongo wake baada ya kumuua mama yake aliyekuwa amembeba wakati wa shambulio hilo.
SOURCE:-BBC SWAHILI. 

No comments: