Saturday, 26 April 2014

KAMA RAFIKI WA KARIBU NYANDU TOZ AZUNGUMZIA FUNUNU JUU YA KUWA Mr BLUE ANATUMIA MADAWA YA KULEVYA.

Taarifa zilizokuwa zikisika Chini kwa chini mtaani kuwa Msanii Mr Blue kwa sasa anatumia Madawa  ya Kulevya,Madawa Ambayo yanayomsababisha Kupungua kwa Ufanisi wake wa Kufanya Kazi na Hata Kubadilisha Muonekano wake na Kuwa tofauti kabisa na Alivyokuwa awali.
Kupitia Kipindi cha TV katika Channel moja maarufu jijini msanii Nyandu Tozi alipokuwa akiizindua Video ya wimbo wake Mpya Ambao unajulikana kwa jina la MAMBO MENGINE BAADAE ambao pia  amemshirikisha Mr Blue katika Chorus.
Ikiwa Kama ni Mfuatiliaji wa karibu wa Muziki Bongo Flava, Basi utakua unajua kuwa Mr Blue na Nyandu Tozi ni Marafiki wa Karibu sana , Kutokana na urafiki na Ukaribu  waliokuwanao basi ni rahisi kujua jambo lolote ambalo linaendelea kwa Rafiki yake,  Kufuatia hilo Nyandu Tozi alipoulizwa kuhusu Mr Blue kutumia Madawa ya Kulevya Alijibu kama ifuatavyo...   
"Unajua Mafans wanashindwa Kutofautisha, kuwa kwa sasa Mr Blue anafanya maisha yake na ana Mtoto  hivyo kwa sasa yeye ni Baba hawezi kufanya Mambo kama aliyokuwa akifanya Zamani, Yule ni mwanangu na Vile vitu hatumii kabisa ni mfumo tu wa maisha ameamua kubadilika"alifunguka NYANDU TOZ.

No comments: