RAHA MASTERS INC & GRAPHIC DESIGNERS.
FIND US ON:-FACEBOOK as Ngessakinollo OR dvjKson on INSTAGRAM.
Wednesday, 14 October 2015
TUME YA UCHAGUZI YAWAKATA RAIA MIL,1 WASIO NA SIFA YA KUSHIRIKI UCHAGUZI 2015.
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi{NEC},Jaji Damian Lubuva.
Tume
ya Taifa ya Uchaguzi , imeyaondoa majina ya wapiga kura zaidi ya
milioni moja kutoka katika orodha ya awali ya watu milioni 23.7
waliojiandikisha awali kwenye Daftari la Kudumu la Wapigakura. Hii
inatokana na kukamilika kwa kazi ya uhakiki wa majina ya watu wote
waliojiandikisha. baada ya uhakiki, imebainika kuwa majina 1,031,769
kutoka miongoni mwa orodha ya awali hawastahili kuwamo kwani baadhi
yao ni majina ya watu waliojiandikisha zaidi ya mara moja, wengine siyo
Watanzania na wapo pia waliokosa sifa nyingine muhimu za kupiga kura,
kwa mujibu wa sheria za nchi. Kwa sababu hiyo, Jaji Lubuva alisema idadi
halisi ya watu watakaokuwa na fursa ya kupiga kura Oktoba 25 ni
22,251,292 kwa Tanzania Bara na wengine 503,193 wa visiwani Zanzibar.
No comments:
Post a Comment