Monday, 16 November 2015

DIAMOND NA VANESSA MDEE WANYAKUA TUZO NYINGINE NDANI YA NIGERIA.


Wakali wawili wa muziki wa Bongo Flava, namzungumzia mwanadada Vanessa Mdee na ‘Icon’ wa Africa Diamond Plutnumz wako nchini Nigeria kwa shughuli za kimuziki.
Mbali na kufanya ‘media tour’, walihudhuria pia hafla ya utoaji tuzo za ‘All Africa music awards’ (AFRIMA) zilizotolewa jana usiku mjini Lagos. Diamond aliyekuwa akiwania ‘tuzo’ hizo, amefanikiwa ‘kuzivuta’ 3 nyumbani Ikiwemo ile ya msanii Bora wa mwaka iliyokuwa ikiwaniwa na Ali Kiba, Davido, Sarkodie, Wizkid, Yemi Alade, Jose Chameleone na Flavour.
Nyingine ‘aliyoibugia’ ni ya msanii bora wa Afrika Mashariki pamoja na wimbo bora wa mwaka. Vanessa yeye alifanikiwa kuinyakua tuzo ya wimbo Bora wa Afro Pop.

Kufuatia kunjinyakulia TUZO hizo tatu Diamond ameandika maneno haya kupitia Instagram yake......

One for my Mother Sandra, one for my Beautiful baby @zarithebosslady and one for my one and Only beautiful daughter! @princess_tiffah ... Bt all these awards are belongs to my Fans because without your Votes i wouldn't have made it, at all!!!...Many thanks and Respect to my Producer @tuddthomas mama Hadija Kopa, my fellow Artists and Media for major Support🙏 and @afrimawards For recognizing my effort🙏 #BongoflavourTotheWorld

 

HALIKADHALIKA VANESSA MDEE "VEE MONEY" NAYE ALIKUWA NA HAYA.......

GLORY TO GOD IN THE HIGHEST! #BestAfricanPop #Hawajui thankyou @nahreel @barnabaclassic and #Tanzania #Africa for letting me sing my song 💜 this one is for you 💜

No comments: